• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

JIJI LA ARUSHA LAGAWA UNGA WA MAHINDI WENYE VIRUTUBISHI KWA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM

Posted on: February 8th, 2023

Na Mwandishi Wetu 

Arusha. 

Halmashauri ya Jiji la Arusha imetoa kiasi cha Shilingi Milioni 33 kwaajili ya kununua unga lishe maalum kwaajili ya watoto wenye mahitaji maalum waliopo mashuleni katika Halmashauri hiyo lengo likiwa ni kuwaongezea afya ya mwili na akili kwa watoto hao.

Akikabidhi unga huo pamoja na vifaa vingine kwenye shule za msingi 9 ambazo zina idadi ya watoto 519 wenye mahitaji maalum Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Bw. Hargeney Chitukuro  amesema Serikali kupitia Halmashauri hiyo imefikia hatua hiyo ya kutoa vyakula vyenye lishe kwa watoto hao wenye mahitaji maalum ili wazidi kukua kiafya na waweze kukuza taaluma zao wawapo madarasani.



"Naishukuru Serikali kwa kuendelea kuwaangalia watoto hawa wenye mahitaji maalumu ili kupata haki zao za msingi ikiwemo elimu. Hawa watoto wanahitaji kukua kiakili na kimwili, pia wanahitaji vifaa mbalimbali vya kuwasaidia watoto hawa". amesema Chitukuro.

"Sisi kama Jiji la Arusha tumesema tutaendelea kuwasaidia watoto hawa katika nyanja mablimbali ikiwemo ya miundombinu mashuleni ili iwe rafiki kwa watoto wetu hawa wenye mahitaji maalum". ameongeza Chitukuro.

Aidha Chitukuro ameeleza kuwa swala kuwanyanyapaa watoto wenye mahitaji maalum halitakuwa sawa maana nao pia wanavipawa kama watu wengine na wanaweza kuwa bora zaidi katika taifa hili na kulisogeza mbele katika hatua mbalimbali.

"Niwaombe wazazi kuendeleza upendo kwa watoto hawa wenye mahitaji maalum tusiwafiche tuwatoe waje wachanganyikane na wengine kwenye kupata elimu bora nao wanayo nafasi ya kuifanyia jambo nchi yao maana wanavipawa vyao". alisema Chitukuro.

Kwa upande wake Afisa Mwandamizi kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Idara ya elimu maalumu Ndg. Seleman Chamshama amesema wao kama Wizara wanaendelea kuhakikisha watoto wote wenye mahitaji maalum hapa nchini wanajiunga na masomo na tayari Serikali inaendelea kuwaboreshea miundombinu ya elimu wawapo mashuleni.

"Yapo mahitaji mengi kwa watoto hawa ikiwamo sare za shule, viatu, madaftari n.k niwaombe watanzania wenzangu wenye kuguswa na hili waweze kuwasaidia watoto hawa ili waweze kupata mahitaji kama walivyo wengine kwasasa Serikali tunahakikisha wanapata elimu ambayo itawasaidia na kukuza vipawa vyao". amesema Chamshama.


"Niwaombe watanzania wengine wenye uwezo waweze kujitoa kuisaidia Serikali kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum maana changamoto ni nyingi Serikali peke yake haitaweza kumaliza ila kwa kushirikiana kwa pamoja tutaweza". aliongeza Chamshama.

Aidha Chamshana aliipongeza Ofisi ya Mkurugenzi Jiji la Arusha kwa kutoa fedha za kuwanunulia chakula chenye lishe watoto wenye mahitaji maalum kwa shule 9 ambazo zote zimepata unga huo pamoja na vifaa vingine ambazo zinajumla ya wafunzi 519 ambao niwanufaika wa msaada huo. Pia amewapongeza wazazi wote waliyo watoa watoto wao ndani na kuwapeleka shuleni kupata elinu.

Akishukuru kwa niaba ya walimu wakuu wa shule hizo 9 Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Kaloleni Mwalimu Miminini Payema ameishukuru Serikali kupitia Mkurugenzi wa Jiji la Arusha kuguswa na kutoa chakula chenye virutubishi vyote vitakavyo saidia watoto kukua kiakili na kimwili.

"Sisi kaloleni mpaka sasa tunao wanafunzi 128 wenye mahitaji maalum tunao wahudumia kuwapatia elimu hii ya msingi niwaombe wazazi wawalete watoto wenye mahitaji maalum ili waje wachanganyikane na wenzao kupata elimu sisi walimu tupo tayari kuwapokea na kuwapatia elimu bora". Amesema Mwl. Payema.



Matangazo

  • KUSITISHWA KWA TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA BONDENI CITY December 06, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI March 14, 2023
  • TANGAZO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KUHUSU KUFUNGULIWA KWA DIRISHA LA MAOMBI YA MIKOPO YA HALMASHAURI July 14, 2022
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA August 11, 2022
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA YATIA FORA UGAWAJI WA MIKOPO, YAMWAGA ZAIDI YA BILIONI 2 ZA MIKOPO KWA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU.

    March 22, 2023
  • JIJI LA ARUSHA LATIA FORA UGAWAJI WA MIKOPO, LAMWAGA ZAIDI YA BILIONI 2 ZA MIKOPO KWA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU.

    March 22, 2023
  • JIJI LA ARUSHA LATIA FORA UGAWAJI WA MIKOPO, LAMWAGA ZAIDI YA BILIONI 2 ZA MIKOPO KWA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU.

    March 22, 2023
  • ZIARA YA KAMATI YA SIASA MKOA WA ARUSHA KATIKA HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHAA

    March 21, 2023
  • Tazama zote

Video

ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa