• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Lucky Vicent wang'ara juma la Elimu

Posted on: May 24th, 2017

Nteghenjwa Hosseah - Arusha

Shule ya msingi Lucky Vicent yaibuka na mshindi wa Jumla Kitaaluma kwa kushika nafasi ya kwanza Kimkoa katika maadimisho ya Juma la Elimu yaliyoadhimishwa katika viwanja vya Arusha School jijini hapa.

Shule hiyo iliyopata na msiba wa wanafunzi 32, walimu 2 pamoja na dereva kutokana na ajali ya Coastal hivi karibuni imefanya vizur katika mitihani ya darasa la saba iliyofanyika mwaka 2016 katika ngazi ya Mkoa na Wilaya hivyo kujinyakulia Kombe pamoja na Cheti.

Akipoka zawadi hizo za Ushindi Mwel Mkuu wa Shule hiyo Bw. Innocent Mushi alisema wanafarijika kupata zawadi hizo ingawa bado simanzi na majonzi yametanda shuleni kwa wanafunzi pamoja na uongozi wa shule hiyo.

“Tunamshkuru Mungu kwa Shule yetu kufanya vizuri na hizi ni jitihada za walimu kufanya kazi kwa bidii pamoja na wafunzi kuzingatia yale wanayofundishwa na walimu wao hakika zawadi hizi zimetupata faraja katika kipindi hiki kigumu tunachopitia.” Alisema Mwl. Mushi.

Katibu Tawala wa Jiji la Arusha Ndg. David Mwakiposa ambaye ndiye mgeni rasmi katika maadhimisho hayo amepongeza shule zote zilizofanya vizuri Kitaaluma kwa mwaka uliopita ikiwa ni pamoja na Walimu na Wanafunzi na pia alitembelea miradi ya kiubunifu inayoendeleza sanaa za wanafunzi ikiwa ni pamoja na kuwawezesha kupata ajira hapo baadae.

Mwakiposa alisema “Taifa lolote haliwezi kuendelea pasipo wananchi wake kuelimika hivyo nichukue fursa hii kuweka msisitizo kwa walimu na viongozi mbalimbali katika sekta ya elimu kufundisha wanafunzi kwa weledi na kutoa elimu bora ili malengo mbalimbali ya kitaaluma yaweze kufikiwa”

Pia aliongeza kwa kusema kuwa amefurahishwa na kuhamasishwa sana katika maonyesho yaliyofanywa na wanafunzi hasa maonyesho ya mafunzo ya kitaaluma, kisayansi na ufundi stadi na kusisitiza kuwa endapo watashirikisha jamii taaluma walizofundishwa na walimu wao na wakiwezeshwa na wadau wa elimu basi Tanzania yetu itapiga hatua kubwa hasa katika suala zima la uchumi wa viwanda.

Miongoni mwa maonyesho yaliyoweza kuonyeshwa na wanafunzi wa kawaida na wenye ulemavu ikiwemo viziwi, matatizo ya akili na wasioona ni pamoja na utaalamu wa kusindika maparachichi na kutengeneza mafuta yanayoweza kutumika kama kilainishi katika karakana za vyuma vyenye kutu na dawa ya ngozi, ujuzi wa kutengeneza dawa ya kung’arishia viatu pamoja na ushonaji wa nguo na vitambaa vya kupambia majumbani.

Pia wanafunzi walionyesha namna ya kuzalisha umeme kwa kutumia nyaya, utengenezaji wa mapambo kwa kutumia shanga zinazotokana na makaratasi na watoto wenye ulemavu wa kusikia wanavyoweza kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)katika kujifunza mambo mbali mbali.

Maadhimisho ya Juma la Elimu hufanyika kila mwaka lengo ikiwa ni kutathimini ubora wa Elimu, kuwatambua waliofanya vizuri kitaaluma na kuonyesha kwa vitendo ubunifu wa wanafunzi na sanaa inavyokua katika sekta ya Elimu.

Mwisho

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa